"VIONGOZI NAO WANATUTAMANI",BATULI


MWIGIZAJI Mkongwe katika tasnia ya filamu bongo Yobnesh Yusuf ‘ Batuli’ ameweka wazi jinsi tasnia ya filamu ilivyo na changamoto nyingi na kujikuta waliomo humo wanakabiriwa na mitihani mingi hata kwa wale ambao wangekuwa msaada kwa kuwasaidia na kusonga mbele kisanaa badala yake uwatolea macho kwa kuwatamani.

 
“Mimi nasema hata bila uoga kabisa sisi kina dada wa Bongo movie tuna mitihani kweli kwani hata hao wakubwa wenyewe ambao ndio msaada ukikutana nao hakuna lolote badala ya kukusaidia kwa kazi yako anakutongoza na shughuli ndio imeisha, mtu anakuita kwa kigezo cha kupitia filamu yako lakini mkiona anakutolea macho anakutaka sasa na wewe filamu hazilipi na unahitaji maisha mazuri,”anasema Batuli.

 
Msanii huyo anasema kuwa anaona wazi kabisa wasanii wa filamu kufanikiwa kwa wakati inakuwa ngumu sana kwani kila mtu anataka kuwa kuwatumia kwa ngono tu kwa sababu anajuwa kuwa wanashida na wanahitaji kutoka, Batuli anasema kuwa pamoja na kuigiza vizuri lakini fursa bado ni chache kwani taasisi kama Basata na nyingine hazijui wajibu wake.

 
Batuli alienda mbali kwa kutolea mifano wasanii kama wa Naijeiria na nchi zilizoendelea wanavyofaidika na kazi zao bila kutegemea Mapedeshee hali iliyopo Bongo hata wale ambao wangekuongoza na kukuonyesha njia wanakutamani na kukutolea macho, pia msanii amedai kuwa tabia hiyo inashamiri kutokana na baadhi ya wasanii wanapokutana na waheshimiwa badala ya kuongelea soko la filamu utanguliza shida zao.



TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments: