NAPE: CCM ITASHINDA KWA ZAIDI YA ASILIMIA 94 UCHAGUZI CHALINZE‏


Nape amesema kampeni zinaenda vizuri lakini wamekumbana na Changamoto za miundombinu ya barabara kutokana na mvua ambazo zinaendelea kunyesha nchini kote, jambo ambalo linaweza kuchangia wagombea kushindwa kuwafikia baadhi ya wananchi katika baadhi ya maeneo ya jimbo hilo, Nape ameongeza kwamba hata hivyo chama hicho kitashinda kwa asilimia 94 katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Aprili 6 Jumapili ijayo.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments: