UTAFITI USIO RASMI:SIKU HIZI WANAWAKE WANAONGOZA KWA VITAMBI NA MATUMBO MAKUBWA



Miaka ya 90 kurudi nyuma ilikuwa nadra sana kukuta mwanamke ana kitambi. Ukimkuta mwanamke anatumbo kubwa wakati huo, lazima atakuwa ana mimba. Hali sasa inatisha. Wanawake wengi wana vitambi kiasi kwamba ni vigumu kutofautisha wenye mimba na wasio kuwa na mimba. Wengi ninao kutana nao barabarani, sehemu za umma, ninaokutana nao maofisini na sehemu mbali mbali nimegundua kuwa kati ya wanawake 10, 7 hadi 8 wana vitambi au matumbo makubwa. Wengine vitambi vyao ni vikubwa na vingine vinakuwa vimevimbiana pembeni yaani upande wa kushoto na kulia ubavuni hivyo kuwa na umbo kama la matumbo ya vyura. La ajabu ni kuwa wanaume wengi sasa hivi hawana vitambi isipokuwa walafi wachache. Kwakuwa zamani tulizoea kuwa vitambi ni kwa wanaume sasa hali imebadilika imekuwa ni wanawake. Nini kimewakuta? Maana wengine ni wasichana wadogo wa shule tayari wanavitambi wakati mwingine utakuta mama ameongozana na binti yake wote wanavitambi. Je kuna namana yoyote ya kuwaokoa? Tuwasaidie maana nadhani hali hiyo itakuwa na athari kiafya kwao mbali ya kuharibu maumbile yao(kupoteza shepu)
Siku utasikia Kila Mwanamke hapa mjini anataka kwenda Gim...
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments: