MTOTO AZALIWA NA UVIMBE WA MKIA KICHWANI MKOANI MARA.. **MSAADA WAHITAJIKA KUYAOKOA MAISHA YAKE

 
MTOTO mchanga wa kike wa eneo la Sabasaba wilayani Tarime  Mkoa wa Mara, Maria Samwel anatakiwa kuhamishiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando ya jijini Mwanza kwa ajili kuondolewa uvimbe wa ajabu uliopo kisogoni.

Mganga Mfawidhi wa Wilaya, Dk. Marco Nega alimwambia  mwandishi wetu  kuwa walifikia uamuzi wa kumhamishia mtoto huyo Hospitali ya Rufaa ya Bugando baada ya kubainika kuwa tatizo lake hilo ni kubwa.
 
“Mtoto huyu alizaliwa na tatizo hilo Julai 14, mwaka huu na atakwenda kutibiwa bure Bugando ili  kuokoa uhai wake,” alisema Dk. Nega.

Mwandishi wetu alizungumza na baba mzazi wa mtoto huyo, Samwel Ryoba, mkazi wa Sabasaba mjini hapa akasema mwanaye anahitajika kufanyiwa upasuaji lakini walichelewa kumpeleka Bugando kutokana na ukata.

‘’Tumechelewa kumpeleka mtoto wetu Bugando ili akaondolewe tatizo hilo kwa kupasuliwa kutokana na kukosa fedha za matumizi wakati tukiwa Mwanza licha ya kuambiwa kuwa mtoto atatibiwa bure.

 Tunaomba msaada wa fedha ya nauli na matumizi mengine kutoka kwa Watanzania angalau shilingi 300,000 kwa maisha ya Mwanza ili tuokoe maisha ya mtoto,‘’ alisema Ryoba.
 

Mama mzazi wa mtoto huo, Kegocha Samwel Ryoba alisema kuwa muda wote wakati wa ujauzito wake alikuwa akihudhuria kliniki hadi hatua ya mwisho ya kujifungua, akashangaa kuona mwanaye ana tatizo hilo na ameomba kusaidiwa.

Wanaoguswa na habari hii wanaweza kutuma fedha kwa namba 0788-218682.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments: