JE, MH. SITTA AMECHUJA AU AMEPAUKA?


Alipokuwa spika wa bunge la 9,alitupa mwamko wa kufuatilia vikao vya bunge.Hasa pale aliporuhusu uundwaji wa kamati ya Mwakyembe iliyochunguza dili la richmond na hatimaye kupelekea kumwagika kwa unga wa EL.Wengi tulijua kuwa mzee amedhamilia kuleta mapinduzi ya kisiasa,kwamba hajali ni mtu wa chama gani,ila anachojali ni viwango na kasi.

Juzi ameaminika na kuchaguliwa kwa kishindo pale bungeni ili kuongoza bunge la katiba,akarudia katika maelezo yake kuwa atakuwa yule yule wa viwango na kasi,wengi wakampigia vigelegele,hata mimi nilifurahi na kurukaruka nikijua jembe limerudi shambani.

Ghafla,akatuacha solemba,akatuduwaza na kutuacha na mshangao mkubwa.Hii ilikuwa ni wiki jana pale alipokubali kanuni zisivunjwe ila zipindishwe.Ilikua amkaribishe JK aanze kuzindua bunge kisha afuatiwe na Warioba.Yeye 6,akapiga tiktaka akiwa amevaa taulo,akamleta kwanza Warioba ! Hii haikuwa kwa bahati mbaya,ila ilikuwa planned kabsaa! Yakawa yaliyokuwa na wote tumeshuhudia na kuhudhunika.Hivi kanuni walizojitungia zitafuatwa kweli kama wa kwanza kuzivunja ni 6 na rais wa nchi!?

Wadukuzi wa siasa zetu wanasema 6 alipewa shinikizo na chama chake ili aruhusu kwanza mwenyemeza wao(mwenyekiti) atanguliwe na Mzee Warioba ili baadae mwenyekiti aje kujibu mapigo.Vipi kama angetangulia mwenyekiti na kisha Warioba angefuata,je,mwenyekiti angesomeka kwa ile hotuba yake kweli?

Kwanini 6 anaonekana kuwa refa anayebeba timu fulani waziwazi? Mmeona kwenye kamati za uongozi alivyoteua?

Je, 6 amechuja au amepauka ?
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments: