DAVID MOYES AJITETEA ..."HATA INGEKUWA NI FERGUSON MSIMU HUU ANGEPATA WAKATI MGUMU"


Meneja wa klabu ya Manchester United, David Moyes amedai kwamba msimu huu wa kwanza kwake hata ungekuwa kwa Sir Alex Ferguson angepata shida kufanya la maana ndani ya msimu ukilinganisha na wachezaji wake wenye umri mkubwa.
“Ukweli nadhai kwamba kama Sir Alex angekua hapa mwaka huu ingekua ngumu kwa Sir Alex pia,nina uhakika hata yeye analijua hilo. Nafikiri watu wanatambua kwamba kuna kikosi ambacho kimepita umri, kwa maana hiyo nadhani ingekua ni msimu mgumu labda kwa yeyote ambaye angekabidhiwa Manchester United mwaka huu,” alisema Moyes

Kauli hiyo ya Moyes imekuja huku Jumamosi hii kundi la mashabiki wa Manchester United likipanga kukodisha ndege itakayopeperusha kibendera chenye maandishi ya kumpinga kocha huyo. Manchester United imekuwa na msimu mbaya kiasi cha mashabiki wa timu hiyo kuanza kulalamika vikali wakimtaka Moyes afutwe kazi.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments: